SIRI YA MAFANIKIO

    Baada ya kusoma kitabu cha  LAW OF MAKING MONEY   kilicho andikwa na BRIAN TRACY    hiki kitabu kinaelezea sheria za kutengeneza fedha au kupata fedha na katika sheria izo ni

   PARKINSON'S LAW : watu wengi sana wanaitumia sheria hii pasipo wenyewe kujua na wengine wanaijua ila awajui kama ni kikwazo kikubwa sana cha mafanikio katika suala zima la fedha katika maisha yao

 Hii sheria inasema kwamba pindi ambapo  kipato cha mtu kinaongezeka na matumizi ya mtu uyo yanaongezeka  Mfano mwalimu ambaye alikua analipwa  shilingi laki tatu na akaona fedha izo ni ndogo na anashindwa kutimiza malengo yake  kwa sababu fedha aliyo kua anaipata inaishia kwenye matumizi  hivyo akaamua kwenda kuongeza elimu ili aweze kupandishiwa mshahara na aweze kutimiza malengo yake na pindi alipo ongeza elimu na mshahara wake ukaongezeka  lakini akashangaa bado  fedha anayo ipata ina isha yote na anashindwa kutimiza malengo yake. Kwa sababu ya sheria  hii ya "Parkinson's law  pindi ambapo samani ya mtu inaongezeka na matumizi ya mtu uyo yana ongezeka au pindi ambapo kipata cha mtu kinaongezeka na matumizi  ya mtu uyo yana ongezeka 

Kwaiyo kipato cha mtu = na matumizi ya mtu uyo

Hivyo hivyo

Pindi ambapo samani ya mtu inaongezeka na matumizi yake yanaongezeka

             Hivyo ili uweze kufanikiwa katika  maisha yako akikisha unaivunja sheria hii ya PARKINSON'S LAW  kwa kupunguza matumizi yako  mfano unaingiza elfu kumi kwa siku akikisha matumizi yako  ni chini ya elfu kumi namaanisha elfu tano na nyingine kawekeze  ila pasipo kufanya ivyo kufanikiwa katika suala zima la fedha itakua ni ngumu sana ivyo akikisha unavunja hii  sheria ndipo uweze kufanikiwa

Pia atakama samani yako ikiongezeka akikisha unapunguza matumizi yako na sio kuongeza matumizi mfano unataka umiliki gari la kifahari kisa umeongezewa mshahara  au unataka kuishi maisha ya kifahari kisa kipato chako kimeongezeka  unatakiwa kupunguza matumizi yako na fedha nyingine  nenda kawekeze kwa kufanya hivyo utaweza kufanikiwa katika suala zima la fedha



Comments

Popular posts from this blog

MAMBO YA KUZINGATIA ILI UWE MFANYA BIASHARA MWENYE MAFANIKIO MAKUBWA

SHERIA ZA BIASHARA